DROO YA KOMBE LA SHIRIKISHO IPO NAMNA HII

LEO Aprili 5 imechezwa droo ya Kombe la Shirikisho pamoja na ile ya ligi ya Mabingwa Afrika.

Kwa upande wa Tanzania wawakilishi ni Simba ambao walikuwa kundi D na kwenye kundi hilo wamepenya sawa na RS Berkane wote wakiwa na pointi 10.

Hivi ndivyo ambavyo kazi itakuwa:-

Simba v Orlando Pirates hii ni ya Afrika Kusini

Pyramids FC V TP Mazembe

Al Masry v RS Berkane

Al Ittihad v Al Ahli Tripoli.

Duru ya kwanza itanza kuchezwa Aprili 17,2022 huku marudiano yakipangwa kufanyika Aprili 24,2022.