ERICKSEN AREJESHWA TIMU YA TAIFA YA DENMARK

CHRISTIAN Ericksen amejumuishwa katika orodha ya kikosi cha timu ya Taifa ya Denmark ambao watacheza mchezo dhidi ya Timu ya Taifa ya Netherlands Machi 26.

Pia atakuwa katika kikosi ambacho kinatarajiwa kucheza dhidi ya Serbia wakiwa nyumbani Machi 29,2022.

Kiungo huyo wa Brentford amerejeshwa kikosini mara ya kwanza tangu alipopata tatizo katika Euro 2022 katika mchezo dhidi ya Finland,Juni 12 2021.