SIMBA YATAJWA KUMALIZANA NA ATAKEYERITHI MIKOBA YA MORRISON

IMEELEZWA kuwa maosi wa Simba wamekamilishw kwa hatua kubwa usajili wa mshambuliaji Moses Phiri raia wa Zambia ambaye anajiunga na Simba msimu ujao akitokea Zanaco ya nchini kwao.

Inaelezwa kwamba, Phiri atakuwa mchezaji wa kwanza kutua Simba kwa wale wapya ambao watajiunga na timu hiyo msimu ujao kutokana na kila kitu kikamilika, anasubiri tiketi tu ya ndege atumiwe ili atue Dar.

 Habari zimeeleza kuwa tayari kila kitu kipo sawa kwa mchezaji huyo kuweza kutua Bongo akiwa ni mrithi wa kiungo mchetuaji, Bernard Morrison.

“Moses Phiri kwa sasa ni mali ya Simba, kulikuwa na mazungumzo ya muda mrefu baina ya uongozi wa Moses Phiri na Simba jambo ambalo makubaliano yalishafikiwa na sasa rasmi mchezaji huyo ni mali ya Simba.

“Mchezaji mwenyewe tayari alishakubali kutua Simba ambapo kigezo kikubwa cha kukamilisha dili la kujiunga na Simba ni kutokana na uwepo wa Wazambia wenzake kama Chama (Clatous) na Bwalya (Rally),” kilisema chanzo hicho.

 Wakala wa mchezaji huyo, Nyambe Nawa kuhusu dili hilo, alisema: “Kuna asilimia kubwa ya Phiri kucheza Tanzania msimu ujao, hivyo ni suala la muda kwa sasa na kila kitu kitakuwa wazi.”