MASTAA HAWA SITA WA SIMBA WAMEITWA STARS

LEO Mei 20,2022 Kocha Msaidizi wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Shadrack Nsajigwa ametangaza orodha ya wachezaji wa timu hiyo watakaoingia kambini.

Wachezaji hao ambao wameitwa kwenye kikosi cha Taifa Stars ambacho kitaingia kambini kujiandaa na michezo ya kufuzu AFCON 2023 wana kazi ya kusaka ushindi kwenye mechi mbili za awali.

Kwa upande wa nyota ambao wametoka Simba ni sita wameitwa ikiwa ni pamoja na:-

 Aishi Manula

 Shomari Kapombe

 Mohamed Hussein

 Kennedy Juma

 Mzamiru Yassin

 Kibu Denis