HUSSEN Masanza, Ofisa Habari wa Singida Black Stars amebainisha kuwa mashabiki katika timu hiyo wanazidi kuongezeka kwa kasi ya ajabu jambo ambalo linamaanisha kukua kwa familia hiyo.
Septemba 30 2025 Singida Black Stars itakuwa na mchezo wa Ligi Kuu Bara ya NBC dhidi ya Mashujaa FC ya Kigoma Uwanja wa KMC Complex saa 8:00 mchana katika msako wa pointi tatu muhimu.
Masanza amesema: “Mashabiki wetu wanaongezeka kwa kasi ya ajabu! Kwa takwimu ambazo bado si rasmi, tunaweza kufikisha zaidi ya mashabiki milioni 10 hivi sasa na familia inazidi kukua kila siku.
“Tunawaona uwanjani, tunaona idadi ya wafuasi ikiongezeka kwenye mitandao yetu na tunaona jinsi msisimko wa mechi zetu ulivyo mitaani.