BEKI YANGA SC MKATABA WAKE UMEKWISHA, ATAJA ATAKAPOSAINI

BEKI wa kazi ndani ya kikosi cha Yanga SC Dickson Job huenda akaongeza kandarasi nyingine ndani ya kikosi hicho. Nyota huyo mkataba wake msimu wa 2024/25 unagota mwisho.

Kwa sasa bado hajaongeza mkataba mwingine na inaelezwa kuwa mazungumzo yameanza kwa pande zote mbili. Juni 29 2025 ulikuwa ni mchezo wa mwisho kwa msimu wa 2024/25 hivyo jambo lake litafanyiwa kazi haraka.

Uongozi wa Yanga SC uliweka kando mazungumzo na wachezaji wengi kutokana na mechi ngumu ambazo zilikuwa juu yao. Kariakoo Dabi Juni 25, Yanga SC 2-0 Simba SC na fainali ya CRDB Federation Cup Juni 29, Yanga SC 2-0 Singida Black Stars.

Mara baada ya Yanga SC kutwaa taji la CRDB Federation Cup, beki huyo aliweka wazi kuwa mkataba wake unaisha hivyo itafahamika wapi atakuwa.

“Kikubwa tusubiri kwa sababu ninakwenda kumaliza mkataba hayo mengine yakiwa sawa kila mtu atajua. Kila kitu kinawezekana kikubwa ni maelewano na mazungumzo mazuri,” alisema Job.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.