BOSI YANGA ASISITIZA KUTOCHEZA KARIAKOO DABI

UONGOZI wa Yanga umeibuka na kusisitiza kuwa hawatacheza mchezo wa Kariakoo Dabi uliopangwa kuchezwa Juni 15, mwaka huu dhidi ya Simba .
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ali Kamwe alisema kuwa wao wanachojua wamebakisha michezo miwili ya Ligi Kuu Bara na siyo mitatu .
“Akili yetu imejikita kwenye kuzimaliza kwa kishindo mechi zetu mbili za Ligi Kuu Bara zilizobaki dhidi ya Tanzania Prisons na Fountain Gate pekee,” alisema Kamwe.