CV YA KOCHA MPYA YANGA IPO NAMNA HII

YANGA SC, imemtangaza Miguel Ángel Gamondi, kuwa kocha mpya wa timu hiyo akichukua mikoba ya Mtunisia, Nasreddine Nabi ambaye waliachana naye hivi karibuni baada ya mkataba wake kufikia tamati.

Gamondi raia wa Argentina, anajiunga na Yanga akiwa mzoefu wa kufundisha soka Afrika kwa zaidi ya miaka 20, huku muda wake mwingi akiutumia kufundisha timu za Ukanda wa Kaskazini mwa Afrika.

Kocha huyo mwenye miaka 56, kabla ya kujiunga na Yanga, timu ya mwisho kufundisha ilikuwa Ittihad Tanger ya Morocco ambapo aliachana nayo Aprili 16, 2022.

Mzaliwa huyo wa Olavarría nchini Argentina, pia ana uraia wa Italia ambapo katika ufundishaji wake, anapendelea zaidi mfumo wa 4-2-3-1.

Akizungumza baada ya kutambulishwa rasmi, kocha huyo alisema: “Mambo Wananchi, mimi ni Miguel Angel Gamondi, kocha kutoka Argentina, nimefanya kazi zaidi ya miaka 20 katika soka la Afrika, nimefundisha timu kama Wydad Casablanca, Mamelod Sundowns, Chabab, Esperance.

“Nilipata mafanikio nikiwa na timu hizo, nina furaha kujiunga na timu kubwa ya Yanga, kwangu naweza kusema ni timu kubwa Afrika, yenye mashabiki wengi.

“Ninaamini tutafanya kazi vizuri na mashabiki, viongozi na wachezaji wote kwa jumla kuleta mafanikio zaidi.

“Nina furaha kujiunga nanyi na tutaonana muda si mrefu. Daima Mbele, nyuma mwiko.”

TIMU ALIZOFUNDISHA

1998–1999       Racing Club de Avellaneda

2000                   Al-Ahly Tripoli (kocha msaidizi)

2001–2002       Burkina Faso (kocha msaidizi)

2002–2003       Wydad Casablanca (kocha msaidizi)

2004                    Espérance (kocha msaidizi)

2005–2006       Mamelodi Sundowns

2007                    Hassania Agadir

2007–2009       Platinum Stars

2010–2011       CR Belouizdad

2011–2012       Ittihad Kalba

2012                    USM Alger

2013–2014       CR Belouizdad

2014                    Al Urooba

2015–2017       Hassania Agadir (Mkurugenzi wa Ufundi)

2017–2019       Hassania Agadir

2020                    Wydad Casablanca

2021–2022       IR Tanger