YANGA 2-0 KAGERA SUGAR

UBAO wa Azam Complex unasoma Yanga 2-0 Kagera Sugar ikiwa ni mchezo wa Ligi Kuu Bara.

Yanga wamepachika mabao hayo kupitia kwa kiungo mshambuliaji Aziz KI ambaye amekuwa kwenye ubora wake.

Lile bao la kwanza ni dakika ya 43 baada ya Fiston Mayele kuchezewa faulo na llle la pili shuti akiwa nje ya 18 dakika ya 45.

Kagera Sugar hawajapiga shuti ambalo limelenga lango kwenye mchezo mpaka sasa