RASMI beki wa kazi ndani ya kikosi cha Simba SC kinachonolewa na Kocha Mkuu, Steve Barker ameanza mazoezi maalumu ili kurejea katika ubora.
Ni Abdulrazack Hamza ambaye alipata maumivu kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga SC uliochezwa Uwanja wa Mkapa.
Anatarajiwa kuwa nje kwa msimu mzima akipambania hali yake ikiwa atatengamaa mapema kuna uwezekano akarejea katikati ya msimu.
Licha ya kuanza mazoezi hayo ni wazi kwamba atakosekana kwenye mchezo ujao wa ligi ugenini ambapo timu ya Simba SC ipo Mwanza.
Machi 19,2026 ni Pamba Jiji FC vs Simba SC mchezo wa NBC Premier League ambapo beki huyo hayupo kwenye mpango wa benchi la ufundi kwa kuwa bado hawajawafiti.
***
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu. Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.
Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.