MTIBWA Sugar 1-3 Singida Black Stars, (SBS) ni matokeo rasmi mchezo wa NBC Premier League uliochezwa mapema leo Februari 22,2026 Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.
Wageni Singida Black Stars wamewatuliza wenyeji kwenye mchezo wa leo ambao ulichezwa saa 8:00 mchana katika msako wa pointi tatu muhimu.
Magoli ya SBS yamefungwa na Ndumumwe Mossi dakika ya 5, Horso Malanga dakika ya 16 na Kennedy Juma dakika ya 58.
Goli pekee la wenyeji Mtibwa Sugar limefungwa na Raizin Hafidhi dakika ya 89. Pointi tatu zimechukuliwa na mgeni.
Mara baada ya mchezo huo Horso alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo akikabidhiwa zawadi na wadhani wa ligi NBC.
***
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu. Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.
Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.