WINGA mpya wa Yanga SC, Allan Okelo amewaaga rasmi wachezaji wa timu ya Vipers United na benchi la ufundi.
Nyota huyo ametambulishwa rasmi kuwa ni njano na kijani usiku wa kuamkia leo Januari 13 2026 ikiwa ni zawadi ya Mapinduzi.
Okelo raia wa Uganda ni miongoni mwa wachezaji waliokuwa AFCON 2025 nchini Morocco na kikosi cha timu ya Taifa ya Uganda kilichoishia hatua ya makundi.
Alianza kikosi cha kwanza kwenye mchezo dhidi ya Tanzania uliokamilika kwa wababe hawa kutoka Afrika Mashariki kugawana pointi mojamoja kwa kufungana goli 1-1.
Akiwaaga wachezaji na benchi la ufundi amebainisha kwamba anawaombea kila la kheri kwenye kutimiza majukumu yao ya kila siku.
“Imekuwa ni muda mzuri kwangu kwa miaka miwili niliyokuwa hapa, wakati mwingine kwa ajili ya changamoto mpya umefika hivyo ninawaombea kila la kheri,”.
Okelo atashuhudia fainali ya NMB Mapinduzi Cup Azam FC vs Yanga SC leo unaochezwa Uwanja wa Gombani, Zanzibar.
***
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu. Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.
Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.