Nigeria vs Tanzania AFCON 2025

Nigeria vs Tanzania ni mchezo mkali unaosubiriwa kwa shauku kwenye mashindano ya AFCON 2025 ikiwa ni hatua ya makundi nchini Morocco.

Tayari mchezo wa ufunguzi ulishachezwa rasmi Desemba 21 ya Jumapili na wenyeji Morocco wakiibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Comoros.

Leo ni kazi ya wawakilishi kutoka Tanzania, Taifa Stars wakiongozwa na nahodha Mbwana Samatta ambaye yupo nchini Morocco.

Ni Nigeria vs Tanzania miongoni mwa kazi ngumu kwa wababe wote wawili ikiwa ni hatua ya makundi.

Miguel Gamondi anatarajiwa kuchanga karata yake ya kwanza leo katika kampeni ya kuwania kufuzu hatua ya robo fainali.

Jumanne, Desemba 23, 2025

Congo Dr vs Benin, saa 9:30 alasiri
Senegal vs Botswana, saa 12:00 jioni
Nigeria vs Tanzania, saa 2:30 usiku
Tunisia vs Uganda, saa 5:00 usiku.

***

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.