Gamondi Ataja Kikosi cha Wachezaji 28 Kwa AFCON 2025, Majina Makubwa Yatupwa

Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Miguel Gamond ametaja kikosi cha wachezaji 28 kitakachopeperusha bendera ya Tanzania kwenye michuano wa kombe la Mataifa Afrika AFCON 2025 huko Morocco ambapo Stars ipo Kundi C, sambamba na Uganda, The Cranes, Nigeria na Tunisia

Nahodha wa Stars, Mbwana Samatta, Simon Msuva, Kibu Dennis na Kelvin John ni miongoni mwa wachezaji walioitwa kuongoza safu ya ushambuliaji huku kinara wa magoli kwenye Ligi Kuu bara, Paul Peter (magoli 5), mshambuliaji wa Simba Sc, Selemani Mwalimu na kiungo wa Young Africans Sc, Mudathir Yahya wakitemwa.