Staa wa Timu ya Taifa ya Ufaransa na Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG), Ousmane Dembélé, ameshinda Tuzo ya Ballon d’Or ya 2025, akiwashinda wachezaji maarufu kama Lamine Yamal wa Barcelona na Mohamed Salah wa Liverpool. Katika msimu wa 2024/25, Dembélé alifunga mabao 37 na kutoa pasi za mwisho 15, akisaidia PSG kutwaa mataji manne muhimu: Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1), Kombe la Ufaransa, UEFA Champions League, na UEFA Super Cup
Ballon d’Or 2025: Dembélé Awashinda Lamine Yamal na Mohamed Salah
