GIBRIL SILLAH AJIUNGA NA ES SÉTIF YA ALGERIA KWA MKATABA WA MIAKA MIWILI

Klabu ya ES Sétif ya Algeria imethibitisha kumsajili rasmi aliyekuwa winga wa Azam FC, Gibril Sillah (26), raia wa Gambia, kwa mkataba wa miaka miwili.

Sillah ameondoka Azam FC baada ya kuitumikia kwa kipindi cha misimu miwili, ambapo aliweka alama ya kudumu akicheza jumla ya mechi 68, kufunga mabao 21 na kutoa asisti 10 kwenye mashindano mbalimbali.

Uhamisho huu unampa nafasi mpya ya kuonesha makali yake katika ligi ya Algeria, huku Azam FC ikipoteza mmoja wa wachezaji wake muhimu wa safu ya ushambuliaji.