SIMBA SC YASAKA KIPA KUMPA CHANGAMOTO CAMARA

SIMBA SC inayonolewa na Kocha Mkuu, Fadlu Davids raia wa Afrika Kusini ipo katika harakati za kumsajili kipa wa JKT Tanzania, Yakoub Seleman katika msimu ujao.

Kipa namba moja kwa sasa ndani ya Simba SC ni Moussa Camara. Ni hati safi 19 amekusanya msimu wa 2024/25 akiwa kipa namba moja mwenye hati nyingi ndani ya ligi namba nne kwa ubora.

Inaelezwa Simba SC wanamtaka kipa huyo haraka na hivi sasa wapo katika harakati za mwishoni za kimyakimya za kumpata Yacoub.

Simba SC kama watampata kipa huyo, basi wataachana na Hussein Abel katika msimu ujao ambaye ni kipa namba tatu wa timu hiyo iliyogotea nafasi ya pili msimu wa 2024/25.

Ipo wazi kwamba mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara ni Yanga SC ambao kipa wao namba moja ni Djigui Diarra chaguo la kwanza la Miloud Hamdi.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.