JEAN AHOUA WA SIMBA SC KATIKA RADA ZA KAIZER CHIEFS

Jean Ahoua kiungo mshambuliaji wa Simba SC anatajwa kuwa kwenye rada za Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini ambayo inatajwa kumfuatilia kwa ukaribu kupata saini yake.

Ahoua ni kinara wa utupiaji mabao ndani ya ligi akiwa amefunga mabao 15 na kutoa pasi 8 za mabao akihusika kwenye mabao 23 kati ya 63 yaliyofungwa na Simba SC.

Taarifa zinaeleza kuwa benchi la ufundi la Kaizer Chiefs linahitaji saini ya mwamba huyo ambaye ni chaguo la kwanza la Kocha Mkuu Fadlu Davids.