VILLARREAL YAKAMILISHA USAJILI WA BEKI WA MAN UTD
Klabu ya Villarreal ya Ligi Kuu Uhispania imekamilisha usajili wa beki Willy Kambwala kwa ada ya uhamisho ya Euro milioni 10 kutoka Manchester United. Kambwala (19) mzaliwa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambaye ameiwakilisha timu ya taifa ya vijana ya Ufaransa amesaini mkataba wa kuwatumikia Nyambizi hao wa Manjano mpaka Juni 2029.