SIMBA YATAMBULISHA BEKI WA KAZI

Klabu ya Simba imemtambulisha beki wa kati, Abdulrazack Mohamed Hamza (23) raia wa Tanzania, akitokea klabu ya Supersport United ya Afrika Kusini kwa kandarasi ya miaka miwili itakayomfanya nyota kuhudumu ndani ya Viunga vya Msimbazi hadi June 2026.
Abdulrazack Hamza ambaye aliwahi kutamba na Mbeya City, KMC na Namungo FC anajiunga na Simba kama mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake.