BRAZIL YAFUZU HATUA YA ROBO FAINALI YA KOMBE LA MATAIFA YA AMERIKA KUSINI

Timu ya taifa ya Brazil imefuzu hatua ya robo fainali ya kombe la Mataifa ya Amerika Kusini licha ya kumaliza hatua ya makundi kwa sare ya 1-1 dhidi ya Colombia katika uwanja wa Levi huko Santa Clara, California Marekani.

Brazil imemaliza nafasi ya pili kwenye Kundi D alama 5 baada ya mechi tatu alama mbili nyuma ya vinara Colombia wenye pointi 7 baada ya mechi 3 ambao pia wamefuzu robo fainali ya Copa America 2024.

Katika mchezo mwingine wa Kundi D, Costa Rica waliomaliza nafasi ya tatu kwa alama nne, imeibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya washika mkia Paraguay wenye pointi sifuri.

FT: Brazil 🇧🇷 1-1 🇨🇴 Colombia
⚽ Raphinha 12’
⚽ Munoz 45+2’

Costa Rica 🇨🇷 2-1 🇵🇾 Paraguay
⚽ Calvo 3’
⚽ Alcocer 7’
⚽ Sosa 55’