KOMBE LA YANGA LATUA KILELE CHA MT. KILIMANJARO

Baada ya msimu 2023/24 kumalizika Mabingwa wa Ligi Kuu ya NBC kwa mara ya tatu mfululizo, Klabu ya Yanga wamepeleka kombe lao walilobeba msimu huu kwenye kilele cha mlima mrefu kuliko yote Barani Afrika, Mlima Kilimanjaro.
Kombe hilo leo Ijumaa Mei 31, 2024 limefika katika kilele cha Mlima Kilimanjaro.
Kabla ya msimu kuanza, Simba SC walifanya uzinduzi wa jezi juu ya kilele cha Mlima Kilimanjaro; uzinduzi uliokwenda sambamba na kampeni ya kibegi.