UWANJA MPYA WA AFCON WAANZA KUJENGWA MKOANI ARUSHA

Serikali kupitia wizara ya Sanaa Utamaduni na Michezo leo Machi 19, 2024 imesaini mkabata wa ujenzi wa Uwanja wa Dokta Samia Suluhu Hassani wenyewe thamani ya shilingi bilioni mia mbili na themanini na Sita ambao utatumika katika michuano ya mataifa Afrika AFCON 2027 inayoandaliwa na nchi za Tanzania, Kenya na Uganda

Akizungumza na waandishi wa habari Waziri wa Michezo Dokta Damasi Ndumbaro amesema Lengo la uwanja huo kujengwa mkoani Arusha ni kuchochea maendeleo ya sekta utalii kupitia michezo.