>

MAPINDUZI CUP FAINALI LEO NI LEO

JANUARI 13 leo ni leo ambapo Michuano ya Mapinduzi Cup inafikia tamati kwa mechi ya fainali kupigwa

Mabingwa watetezi ambao ni Mlandege kucheza na Simba SC ambao wametinga hatua ya fainali 2024.

Ni bao la Fabrince Ngoma lilileta nongwa dakika za lala salama na kupelekea mikwaju ya penalti.

Singida Fountain Gate 2-3 Simba kwenye penalti baada ya kufungana bao 1-1 kwenye dakika 90 za jasho.

Mlandege wao walitinga hatua hii kwa ushindi mbele ya APR na Simba iliwaondoa Singida Fountain Gate.

Fainali hii inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa ambapo Mlandege wao ni mabingwa watetezi na Simba wanalipigia hesabu taji hilo.

Ipo wazi kuwa Mlandege wamefunga jumla ya mabao mawili kuanzia hatua ya makundi sawa na yale waliyofungwa huku Simba ikifunga jumla ya mabao 7 na kufungwa mabao mawili.