“Tutautumia Uwanja wa Black Rhino wa Karatu mpaka pale uwanja wa CCM Liti wa mjini Singida utakapokuwa tayari tena kwa matumizi ila kazi kubwa itafanyika kwenye mechi zetu zote kutafuta ushindi.
“Tuna mechi mbili ambazo zipo karibu hizo tutatumia uwanja huo itakuwa ni Desemba 11 dhidi ya KMC na Desemba 15 dhidi ya Arusha FC mchezo wa Kombe la Azam Sports Federatio,”.
Taarifa ambayo imetolewa na Singida Fountain Gate Desemba 10 imeeleza kuwa mapato yote ya klabu katika mchezo dhidi KMC yatakuwa ni maalumu kuchangia kwenye kusaidia ndugu walioathirika na mafuriko, Hanang, Manyara.