>

ALIYEWAVURUGA WAARABU KWA MKAPA ATOA TAMKO ZITO

KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Pacome aliyewavuruga namna anavyopenda Waarabu Al Ahly kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika ameweka wazi kuwa watapambana kupata matokeo kwenye mechi zinazofuata Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi.

Yanga iligawana pointi moja kwenye mchezo wa kwanza wakiwa nyumbani hatua ya makundi kwa kufungana bao 1-1 dhidi ya Waarabu wa Misri Al Ahly huku bao la kufutia machozi likifungwa na Pacome dakika ya 90.