RATIBA YA MAKUNDI CAF: SIMBA YAPEWA WYDAD, YANGA USO KWA USO NA AL AHLY

DROO ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika imekamilisha ambapo vigogo 16 wa Afrika wamebaini wapinzani wao huku Simba na Yanga wakikwepana.

Simba SC imepangwa Kundi B sambamba na Wydad Casablanca ya Morocco, ASEC Mimosas ya Ivory Coast na Jwaneng Galaxy ya Botswana.

Kwa upande wake Yanga SC imepangwa Kundi D sambamba na Mabingwa watetezi Al Ahly ya Misri, CR Belouizdad inayonolewa na Kocha wa zamani wa Simba SC, Sven Vandenbroeck na Medeama ya Ghana.

KUNDI A:

• Mamelodi Sundowns ??
• Pyramids FC ??
• TP Mazembe ??
• FC Nouadhibou ??

KUNDI B:

• Wydad AC ??
• Simba SC ??
• ASEC Mimosas ??
• Jwaneng Galaxy ??

KUNDI C:

• ES Tunis ??
• Petro Luanda ??
• Al Hilal ??
• Etoile Sahel ??

KUNDI D:

• Al Ahly ??
• CR Belouizdad ??
• Yanga SC ??
• Medeama ??