“Kuna wachezaji watatu ambao hawajatajwa popote kwa sasa hao watatambulishwa siku ya Singida Fountain Gate na itakuwa ni zawadi kwa mashabiki wa timu,” ilieleza taarifa hiyo.
“Maandalizi yanakwenda vizuri na kutakuwa na mambo matano ambayo yatafanyika ikiwa ni pamoja na utambulisho wa wachezaji na benchi la ufundi kwa msimu mpya wa 2023/24.
“Pia kutakuwa na mechi za kirafiki kwa timu ya Wanawake na ile ya Wanaume hivyo mashabiki wajitokeze kwa wingi kushuhudia burudani,” amesema Masanza.
Timu hiyo ipo chini ya Kocha Mkuu, Hans Pluijm ambaye anaendelea na maandalizi kwa ajili ya msimu wa 2023/24.