MWAMBA ALIYEKUWA ANAWINDWA NA YANGA NI MNYAMA

RASMI Fabrice Ngoma ambaye ni kiungo ametambulishwa kuwa mali ya Simba.

Nyota huyo anakuja kuungana na wachezaji wengine kwa ajili ya kupambania malengo ya msimu wa 2023/24 na timu imeweka kambi Uturuki akijua kuwa ubingwa msimu wa 2022/23 upo kwa Yanga.

Alikuwa anatajwa kuwa kweye rada za Yanga pamoja na Azam FC ila Simba wanatajwa kufanikisha mpango wao wa kuinasa saini yake.

Ni amenunuliwa kutoka kutoka Al-Hilal ya Sudan hivyo anakuja kuanza changamoto mpya ndani ya Ligi Kuu Bara ambapo wanatarajia kuanza na Singida Fountain Gate kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii, Tanga.