WAWILI SIMBA WAMEGOTA MWISHO

BEKI wa Simba Mohamed Outtara hatakuwa sehemu ya kikosi hicho kwa msimu wa 2023/24.

Nyota huyo alikuwa kwenye kikosi kilichopoteza Ngao ya Jamii mbele ya watani za jadi Yanga uliochezwa Uwanja wa Mkapa.

Katika mchezo huo Yanga iliibuka na ushindi wa mabao mawili yote yakifungwa na Fiston Mayele ambaye alimtungua Beno Kakolanya.

Ni Pape Sakho alianza kuwatungua Yanga kipindi cha kwanza lakini mambo yalikuwa magumu kwao kushinda mchezo huo.

Beki huyo ni msimu mmoja ametumika ndani ya kikosi cha Simba kinachonolewa na Kocha Mkuu Robert Oliveira.

Anakuwa nyota wa pili kupewa Mkono wa kwa heri Juni 20 wa kwanza ni Victor Ackpan ambaye ni kiungo.

Ni Agustino Okra alifungua njia kwa nyota waliopewa Mkono wa kwa heri ndani ya Simba