BAO LA MAYELE LASEPA NA TUZO CAF

BAO alilopachika mwamba Fiston Mayele kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya US Monastir limechaguliwa kuwa bao bora kwa mzunguko wa tano.

Nyota huyo mtambo wa mabao alipachika bao hilo kwenye mchezo uliochezwa Machi 19,2023 Uwanja wa Mkapa.

Pasi ya mshikaji wake Kennedy Musonda ilikutana na Mayele aliyekuwa nje kidog ya 18 akaachia shuti kali lililomshinda mlinda mlango wa US Monastri.

Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 US Monastir na kusepa na pointi zote tatu mazima ikiwa nyumbani.

Inafikisha pointi 10 ikiwa ni namba moja kwenye msimamo hatua ya makundi.