YANGA YAICHAPA KICHAPO ZALAN KWA MKAPA

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Bara, Yanga ambao wanaiwakilisha Tanzania kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika wameibuka na ushindi mkubwa wa mabao 5-0 dhidi ya Zalan FC.

Ni kwenye mchezo wa pili wa Ligi ya Mabingwa Afrika na kuwafanya washinde kwa jumla ya mabao 9-0 dhidi ya Zalan FC ukiwa ni ushindi mkubwa kutokea kwa hivi karibuni.

Leo Septemba 17, Uwanja wa Mkapa ni mabao ya mzawa Farid Musa aliyefungua ubao wa kufunga kisha Aziz KI na Fiston Mayele akatupia mabao matatu.