>

KUWAONA MAYELE,AZIZ KI, DUBE NI BUKU TANO

 SEPTEMBA 6, Uwanja wa Mkapa, ni Dar Dabi kati ya Yanga v Azam FC, ambapo kuwaona mastaa wa timu hizo mbili wakisaka ushindi ikiwa ni pamoja na Dennis Nkane, Fiston Mayele, Bernard Morrison na Aziz Ki kwa Yanga ni buku tano, (5,000).

Kwa upande wa Azam FC ambao ni wageni kwenye mchezo huo wapo nyota ambao ni Prince Dube, Daniel Amoah, Agrey Morris na Ibrahim Ajibu.

 Kiingilio kwenye mchezo huo ni 5,000 kwa viti vya machungwa, bluu na kijani, VIP A & B ni 10,000 na VIP A ni 15,000.

Timu zote mbili zinatarajiwa kukutana uwanjani ambazo ni dakika 180.

Azam FC imeshinda mchezo mmoja na kuambulia sare moja huku kwa upande wa Yanga wakiwa wameshinda mechi zote mbili.