>

SAUTI:AZAM FC WATAMBIA BEKI WAO WA KUPANDA NA KUSHUKA

NATHANIEL Chilambo nyota aliyekuwa anacheza ndani ya kikosi cha Ruvu Shooting msimu wa 2022/23 atakuwa ni mali ya Azam FC ambayo itakwenda kushiriki mashindano ya kimataifa baada ya kumaliza msimu ikiwa nafasi ya tatu. Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Azam FC,Zakaria Thabit amesema kuwa bado wataendelea kushusha wachezaji wengine.