Home Sports HIZI HAPA REKODI ZA MAKIPA WANAOWANIA TUZO BONGO

HIZI HAPA REKODI ZA MAKIPA WANAOWANIA TUZO BONGO

LEO ni leo itakuwa kwa kuwa ni siku ya ugawaji wa tuzo kwa wanamichezo baada ya kukamilisha msimu wa 2021/22 ambapo mabingwa ni Yanga.

Julai 7 zinatarajiwa kufanyika tuzo hizo kwenye Ukumbi wa Rotana Hotel, huku moja ya kipengele ambacho kinatazwa kwa ukaribu ni upande wa mlinda mlango.

Hapa tunakuletea rekodi za mastaa hao watatu waliopenya kuwania tuzo hiyo ya kipa bora zilizoandaliwa na Bodi ya Ligi Tanzania ambapo mmoja atasepa nayo jumlajumla namna hii:-

Manula

Air Manula, Aishi Manula yeye ni kipa namba moja ndani ya kikosi cha Simba akiwa anaitetea tuzo yake ambayo alisepa nayo msimu wa 2020/21.

Msimu huu amecheza mechi 21 na kuyeyusha dk 1,890 akiwa hajafungwa kwenye mechi 11 na ametunguliwa mabao 11.

Mechi zake za ushujaa

Biashara United 0-0 Simba

Dodoma Jiji 0-1 Simba

Simba 1-0 Polisi Tanzania

Simba 0-0 Coastal Union

Simba 1-0 Namungo

Simba 0-0 Yanga

Mtibwa Sugar 0-0 Simba

Simba 1-0 Prisons

Yanga 0-0 Simba

Simba 1-0 Mbeya Kwanza

Simba 2-0Kagera Sugar

Hapa alipata tabu

Ruvu Shooting 1-3 Simba

Simba 2-1Geita Gold

KMC 1-4 Simba

Simba 2-1 Azam FC

Mbeya City 1-0 Simba

Kagera Sugar 1-0 Simba

Coastal Union 1-2 Simba

Namungo 2-2 Simba

Simba 4-1 Ruvu Shooting

Azam FC 1-1 Simba

Diarra

Kipa namba moja wa Yanga Diarra Djigui ikiwa ni msimu wake wa kwanza kuitumikia timu hiyo ambayo imesepa na ubingwa wa Ligi Kuu Bara.

Rekodi zinaonyesha kwamba amecheza jumla ya mechi 22 na hajafungwa kwenye mechi 15 akiwa ametunguliwa mabao 7 kwenye dk zake 1,944.

Clean sheet zake

Kagera Sugar 0-1 Yanga, dk 90

Yanga 1-0 Geita Gold,dk 90

KMC 0-2 Yanga,dk 90

Yanga 2-0 Azam FC,dk 90

Mbeya Kwanza 0-2 Yanga, dk 90

Simba 0-0 Yanga,dk 90

Mtibwa Sugar 0-2 Yanga,dk 90

Yanga 3-0 Kagera Sugar,dk 90

Geita Gold 0-1 Yanga,dk 90

Yanga 2-0 KMC,dk 90

Yanga 0-0 Simba,dk 90

Ruvu 0-0 Yanga,dk 90

Yanga 0-0 Prisons,dk 54

Dodoma Jiji 0-0 Yanga, dk 90

Yanga 4-0 Mbeya Kwanza,dk 90

Mishale ilipenya

Yanga 3-1 Ruvu Shooting,dk 90

Namungo 1-1 Yanga,dk 90

Prisons 1-2 Yanga,dk 90

Yanga 2-1 Biashara United,dk 90

Azam FC 1-2 Yanga,dk 90

Yanga 2-1 Namungo,dk 90

Mbeya City 1-1 Yanga

Aboubhakari

Khomeny Aboubhakari wa Geita Gold inayonolewa na Kocha Mkuu, Felix Minziro yeye ni miongoni mwa wanaowania tuzo hii.

Rekodi zinaonyesha kuwa ni mechi 14 ambazo amekaa langoni ambazo ni sawa na dk 1,260,hajafungwa kwenye mechi 5 na amefungwa jumla ya mabao 10 kwenye mechi 9 alizotunguliwa.

Hizi hapa 9 alitunguliwa

Yanga 1-0 Geita Gold

Geita Gold 1-1 Mbeya City

Azam FC 1-0 Geita Gold

Kagera Sugar 1-2 Geita Gold

Simba 2-1 Geita Gold

Geita Gold 2-1 Ruvu Shooting

Geita Gold 1-1 Mbeya Kwanza

Dodoma Jiji 1-1 Geita Gold

Geita Gold 1-1 Simba

Clean sheet zake

 Geita Gold 2-0 Biashara United

Geita Gold 1-0 Prisons

Biashara United 0-0 Geita Gold

Mtibwa Sugar 0-2 Geita Gold

Mbeya Kwanza 0-1 Geita Gold

Previous articleMSELELEKO WALIOUPATA AZAM FC KUMNASA MR HAT TRICK HUU HAPA
Next articleSAUTI:KIKOSI KIPYA CHA YANGA CHEKI KILIVYO