HII HAPA RATIBA YA ANGA LA KIMATAIFA, AZAM FC, SIMBA, YANGA SC, SINGIDA BS

WIKIENDI imechangamka kwenye anga la kimataifa kutokana na timu zote nne kutoka Tanzania kuwa katika kazi.

Ijumaa, Uwanja wa 11 de Novembro, Wiliete Sports vs Yanga SC, saa 12:00 jioni.

Simba SC Jumamosi Septemba 20 itakuwa uwanjani kumenyana na Gaborone United saa 2:00 usiku.

Yanga SC na Simba SC ni katika Ligi ya Mabingwa Afrika ikiwa ni hatua ya awali.

Azam FC wapo Sudan Kusini watacheza dhidi ya Al Merriekh Bentiu Septemba 20 saa 11:00 jioni.

Singida Black Stars wapo Reanda watakuwa na mchezo dhidi ya Rayon Sports Septemba 20 2025.

Azam FC na Singida Black Stars ni katika Kombe la Shirikisho Afrika.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.