MBEYA DAY NI LEO KUNOGESHWA NA MECHI KALI DHIDI YA AZAM FC

PAZIA la Ligi Kuu Tanzania Bara ya NBC ambayo ni namba nne kwa ubora linakaribia kufunguliwa ikiwa ni siku zinahesabiki kwa kuwa Septemba 17 kazi inatarajiwa kuanza.

Leo kuna tamasha kubwa nyanda za juu Kusini, ambapo Mbeya City iliyorejea kwa mara nyingine ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo ni namba nne kwa ubora Afrika watakuwa na jambo lao.

Mbey City, The Purple Nation,  Uwanja wa Sokoine, Mbeya watafanya utambulisho wa kikosi chao cha msimu wa 2025/2026 unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Miongoni mwa wachezaji waliopo Mbeya City ni kipa wa zamani wa Simba SC na Yanga SC, Beno Kakolanya ambaye yupo hapo kwa mara nyingine tena katika kutimiza majukumu yake.

Kutakuwa na mchezo mkali wa kirafiki kati ya wenyeji Mbeya City dhidi ya matajiri wa Dar, Azam FC ambao unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Sokoine, Mbeya.

Kocha Msaidizi wa Mbeya City Mussa Rashid ameweka wazi kuwa wapo tayari kwa mchezo huo na watatoa burudani nzuri kwa mashabiki watakaojitokeza.

Hasheem Ibwe, Ofisa Habari wa Azam FC ameweka wazi kuwa wapo tayari kwa mchezo na wapinzani wao Mbeya City wamefanya makosa kuichagua Azam FC kwa kuwa ina hasira kutafuta matokeo hata kama imealikwa.

Mgeni rasmi kwenye tamasha hilo ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Beno Malisa atashuhudia burudani zote kwenye tukio hili kubwa.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.