AZAM FC matajiri wa Dar wamepanga kutumia michuano ya Kimataifa Afrika (Chan) kwa ajili ya kufanya usajili wa msimu ujao wa 2025/26.
Ipo wazi kwamba CHAN mchezo wake wa ufunguzi unatarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa, Agosti 2 kati ya Tanzania ambao ni wenyeji itakuwa dhidi ya Burkina Faso.
Tayari Azam FC imekamilisha usajili wa kipa mzawa Aishi Manula ambaye alikuwa ndani ya kikosi cha Simba SC amerejea kwa mara nyingin ndani ya kikosi hicho kwa changamoto mpya 2025/26.
Mkuu wa Kitengo cha Habari cha Azam, Thabit Zakaria amesema kuwa wamepanga kusajili wachezaji wa kigeni wenye uzoefu wa kimataifa wakati wakijiandaa na Kombe la Shirikisho Afrika.
“Hatutaki kukurupuka katika usajili wetu, hivyo tutazingatia uzoefu wa wachezaji wa kucheza michuano ya kimataifa, hivyo tutatumia Chan kufanya skauti, “amesema Zakaria.
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.