Yanga SC vs Silver Strikers CAF Champions League, mashabiki waachiwa mechi

KUELEKEA kwenye mchezo wa marudiano CAF Champions League, Oktoba 25 2025 uongozi wa Yanga SC umeweka wazi kuwa mechi hiyo itakuwa mikononi mwa mashabiki baada ya kuomba wapewe hilo jukumu.

Hiyo imetokana na mashabiki wengi kufunga safari kuelekea nchini Malawi kuishangilia timu hiyo Oktoba 18, 2025 kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Bingu matokeo yaliposoma Silver Strikers 1-0 Yanga SC.

Yanga SC inahitaji ushindi wa angalau goli 2-0 katika mchezo wa Oktoba 25,2025, Uwanja wa Mkapa huku mashabiki wakiombwa kuwa wastaarabu na wasifanye vurugu yoyote ile wala kuwasha moto wakiwa uwanjani.

Ali Kamwe Ofisa Habari wa Yanga SC amesema kuwa wanachama wa Yanga SC waliomba mechi ya Jumamosi kusiwe na viingilio jambo ambalo limefanyiwa kazi na uongozi kwa umakini mkubwa na kuamua iwe hivyo.

“Tumepokea maoni mengi kutoka kwa Wanachama wetu wakiuomba uongozi wa Yanga kuwa mechi ya jumamosi usiwe na viingilio, tuwaachie wao mchezo huu na tuwape nafasi ya wao kuisapoti timu yetu na kuivusha kwenda hatua ya makundi.

“Tayari uongozi wetu umekutana na kujadili maoni haya ya wanachama na kimsingi wamelipokea, wamekubaliana na kulipitisha ombi hili la Wanachama wetu. Hivyo ombi limekubaliwa na mashabiki wawe makini kwenye mchezo wetu wasilete vurugu.

“Ikitokea ni shabiki wa Mtibwa Sugar, Mbeya City ama timu yoyote amekuja usimsumbue muache aangalie mpira apate burudani lakini akija a malengo tofauti huyo lazima aondolewe kwa kuonyeshwa mlango wa kutokea,” Ally Kamwe.

***

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.