MZIZE KULIPWA MSHAHARA MREFU YANGA SC

MSHAMBULIAJI wa Yanga SC, Clement Mzize kuna uwezekano mkubwa akabaki ndani ya kikosi hicho kwa msimu wa 2025/26 na atakuwa anakunja mshahara mrefu kwa mwezi.

Taarifa zilikuwa zinaeleza kuwa Mzize kuna timu ambazo zinahitaji huduma yake kutoka Ulaya jambo ambalo lilikuwa linasubiriwa ni kuisha kwa mashindano ya CHAN. Wakati mashindano yanaendelea Tanzania imeishia hatua ya robo fainali.

Taarifa zinaeleza kuwa Mzize ambaye kwenye ligi alifunga mabao 14 akiwa mshambuliaji mzawa mwenye mabao mengi katika CHAN a2024 alifunga mabao mawili huenda hataondoka kwa ajili ya changamoto mpya atasalia Yanga SC.

Mshambuliaji huyo inatajwa kuwa alikaa kikao na viongozi wa Yanga SC wakifikia makubaliano ya kuongeza mshahara wake na posho.

Kwa mujibu wa chanzo cha Habari kutoka ndani ya Yanga, mshambuliaji huyo amefanyiwa maboresho ya mshahara wake ambao unafikia zaidi ya milioni 45 atakaoupata hadi msimu 2026/27.

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga, Ali Kamwe alizungumzia hilo kwa kusema kuwa “Zipo ofa mbili kutoka ndani nan je ya Afrika zikimuhitaji Mzize, Uongozi unazipitia hivi sasa lakini ikumbukwe bado mchezaji wa Yanga hadi 2027.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.