YANGA SC YAANZA KUISOMA SIMBA SC KUELEKEA KARIAKOO DABI

MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga SC wameanza kupiga hesabu kuelekea mchezo wa Kariakoo Dabi dhidi ya Simba SC.

Mchezo huo unasubiriwa kwa shauku kubwa unatarajiwa kuwa na ushindani ndani ya dakika 90 kwa wababe hao katika uwanja kusaka ushindi.

Inaelezwa kuwa tayari Kocha Mkuu wa Yanga SC, raia wa Ufaransa, Romain Folz amekabidhiwa video za michezo ya mwisho ya Ligi Kuu Bara ya wapinzani wao Simba SC ambao kwa sasa wapo nchini Misri kwa kambi kuelekea msimu mpya.

Kwa mujibu wa chanzo kutoka ndani ya Yanga SC, video zaidi ya mbili tayari amepatiwa kocha huyo haraka tayari ameanza kuzipitia pamoja na benchi lake jipya la ufundi kuelekea msimu mpya.

Chanzo hicho kilisema kuwa lengo la kupitia video hizo ni kwa ajili ya kuziona mbinu za Kocha Mkuu wa Simba SC, Fadlu Davids na wachezaji hatari wa kuchungwa kabla ya kukutana nao Ngao ya Jamii Septemba 16 2025.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.