WAKATI Tanzania Agosti 16 2025 kwenye mchezo wa CHAN 2024 ikishuhudia ubao wa Uwanja wa Mkapa ukisoma Afrika ya Kati 0-0 Tanzania, kiungo Feisal Salum amebainisha kuwa watapambana katika hatua ya robo fainali kupata matokeo mazuri.
Mchezo huo uliopita hatua ya makundi ulikuwa wa kwanza kwa Tanzania kugawaa pointi mojamoja. Katika mechi tatu ambazo zilipita za makundi Tanzania ilishinda zote ikikusanya pointi 9.
Baada ya mechi nne, Tanzania inaongoza kundi B ikiwa na pointi 10 itacheza na Morocco hatua ya robo fainali mchezo unaotarajiwa kuchezwa Agosti 22, 2025 Uwanja wa Mkapa.
Nyota huyo ambaye alichaguliwa kuwa mchezaji bora baada ya mchezo alibainisha kuwa wanatambua kuna kazi kubwa mbele yao hivyo watapambana kuwa bora zaidi.
“Kwenye mchezo wetu uliopita haikuwa shida katika kutafuta matokeo kwa kuwa tulienda na game plan yetu ya kile ambacho tulifundishwa mazoezini. Ambacho walifanya wapinzani wetu ni kuziba nafasi ambazo tulizifanyia mazoezi. Mimi mchezaji katika matokeo tuliyopata hatujaridhika.
“Tulitegemea matokeo kwenye mchezo wetu. Wenzetu walituheshimu na kuja kwa umakini. Mchezo huu umepita tunaangalia mechi zijazo hatua ya robo fainali. Tunaamini tutapambana kufanya vizuri zaidi, “ amesema Fei Toto
Kocha Mkuu wa Tanzania, Hemed Suleman ameweka wazi kuwa makosa yaliyopita watafanyia kazi ili kupata matokeo kwenye mechi zijazo.
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu. Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.
Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.