MSHAMBULIAJI MPYA SIMBA SC JONATHAN SOWAH ATUMA UJUMBE

MSHAMBULIAJI mpya wa Simba SC 2025/26 Jonathan Sowah raia wa Ghana ametuma ujumbe kwa mashabiki kwa kubainisha kuwa watafurahi msimu mpya. Nyota huyo yupo kambini nchini Misri chini ya Kocha Mkuu, Fadlu Davids.

Sowah alitambulishwa ndani ya kikosi cha Simba SC akitokea Singida Black Stars. Msimu wa 2024/25 alifunga jumla ya magoli 13. Katika mabao hayo aliwafunga watani wa jadi Yanga SC kwenye mchezo wa ligi uliochezwa Uwanja wa KMC Complex.

“Mimi Jonathan Sowah ni Simba mweusi. Ninapenda kuwaambia mashabiki wa Simba SC kuwa watafurahi. Kwa kila shabiki ambaye atakuja uwanjani na yule ambaye atakuwa nyumbani hakika atafurahi.

“Kuna mengi ambayo tunaamini tutafanya. Ushirikiano mkubwa kwa wachezaji na benchi la ufundi. Hakika kila mmoja atafurahi, mashabiki tuzidi kuwa pamoja.”

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.