KIUNGO AZIZ ANDAMBWILE BADO YUPO JANGWANI

NI majeraha ambayo yalifanya asionyeshe ubora wake akiwa katika uwanja msimu wa 2024/25 na alipata maumivu makubwa kwenye mchezo dhidi ya TaboraUnited alipokomba dakika 10 pekee, Uwanja wa Azam Complex.

Ilikuwa ni Novemba 6 2024 zama za Kocha Mkuu, Miguel Gamondi.

Anaitwa Aziz Andambilwe alicheza jumla ya mechi tano za ligi akikomba dakika 125, hakufunga wala kutoa pasi ya bao kiungo ambaye alikuwa anacheza nafasi ya beki wakati mwingine.

Katika mchezo dhidi ya JKT Tanzania uliochezwa Uwanja wa Azam Complex alikomba dakika 90 na ubao ukasoma Yanga SC 2-0 JKT Tanzania.

Ilikuwa ni Oktoba 22 2024, mwamuzi alikuwa Ahmed Arajiga, Azam Complex . Ameongeza mkataba wa miaka miwili bado yupo Jangwani kijana mpaka 2027.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.