RASMI Simba SC imefanya utambulisho wa mchezaji wa kwanza kuelekea msimu wa 2025/26. Hii ni baada ya sanduku la usajili kupatikana kwenye kina kirefu cha bahari ya Hindi.
Baada ya usajili kufunguliwa Simba SC ilikuwa kimya huku watani zao wa jadi wakitambulisha wachezaji wapya wa kazi kwa ajili ya msimu mpya unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.
Anaitwa Rushine De Reuck ambaye ni beki aliyewahi kucheza Mamelod Sundowns ya Afrika Kusini anakotokea Kocha Mkuu wa Simba SC, Fadlu Davids.
Haya ni maandailizi ya Simba SC ikiwa ni kuelekea Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo ni namba nne kwa ubora Afrika.
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu. Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.
Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.