UBINGWA WA CECAFA WALETA MATUMAINI KUELEKA CHAN, FA AFUNGUKA

NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamis Mwinjuma maarufu kwa jina la FA amebainisha kuwa timu ya Tanzania ipo vizuri. Hayo alisema mara baada ya Tanzania kupata ushindi dhidi ya Uganda. Mwinjuma amesema kwenye mpira wa miguu lolote linaweza kutokea.

Ikumbukwe kwamba kwenye mashindano maalumu ya CECAFA ambayo yalishirikisha timu tatu, Tanzania, Uganda na Senegal bingwa ni Tanzania.

Katika mchezo wa Julai 27 2025 uliochezwa Uwanja wa Black Rhino baada ya dakika 90 Tanzania ilipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Senagal.

FA alisema: “Timu ipo tayari sijaona timu nyingi zikishiriki.Ila kwa timu ambazo zimeshiriki Uganda na Senegal nit imu nzuri. Kwa sasa tuna nafasi kitwakimu kuchukua ubingwa huu.

“Kupata matokeo mbele ya Uganda, Senegal hapo unaona kwamba tumechukua CHAN ya huku Karatu. Bado CHAN 2024 ya Afrika nzima ambayo tunakwenda kushiriki. Tuna nafasi kubwa kuchukua kombe hili kuliko wakati wowote ule ila kwenye mpira lolote linaweza kutokea,”.

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo na Moyo Wangu Unavuja Damu.  Kuvipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371.

Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Msichana wa Maisha Yangu, jiandae kuipata.