HUYU HAPA KAPEWA MAJUKUMU YA USAJILI SIMBA SC

WAWAKILISHI wa Tanzania kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba SC msimu wa 2025/26 wameweka wazi kuwa mpango kazi wa kufanya usajili upo chini ya Kocha Mkuu, Fadlu Davids.

Ikumbukwe kwamba msimu wa 2023/24 Simba SC iligotea nafasi ya tatu kwenye msimamo ikapeperusha bendera kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.

Kwa msimu wa 2024/25 iligotea kuwa mshindi wa pili Kombe la Shirikisho Afrika na bingwa alikuwa ni RS Berkane.

Kwa mujibu wa Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano Simba SC Ahmed Ally ameweka wazi kuwa mpango mkubwa kwa msimu ujao ni kufanya vizuri zaidi na watafanya usajili makini.

“Kwenye kufeli msimu uliopita ni sehemu ya matokeo kwa kuwa bado tunajenga timu hilo lieleweke na mashabiki wasikate tamaa wala wasiishiwe pawa. Kikubwa ni mshikamano na kuendelea kufanya kazi kwa ushirikiano.

“Kwa msimu huu asilimia kubwa suala la usajili litakuwa mikononi mwa Kocha Mkuu, Fadlu Davids, yeye atasimamia kila kitu na viongozi watakamilisha mpango kazi.”

Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.