FADLU Davids, Kocha Mkuu wa Simba SC amekabidhiwa rungu la kufanya maamuzi kwa wachezaji ambao wanapaswa kuondoka katika kikosi hicho na wale ambao watabaki kwa msimu wa 2025/26.
Miongoni mwa wachezaji ambao Fadlu amebainisha kwamba anahitaji wabaki inaelezwa ni beki Mohamed Hussen ambaye mkataba wake umeisha akiwa anatajwa kuwa katika rada za Yanga SC.
Kocha huyo alifanya kikao na Rais wa Simba SC, Mo Dewji hivyo kuna uwezekano mkubwa akaendelea kuwa katika kikosi hcho kwa msimu mpya wa 2025/26.
Muda mfupi walipokutana Mo aliandika namna hii: “Tulia. Tathmini. Panga upya. Nimefurahi kuwa na mazungumzo ya maana na Kocha Fadlu katika msimu wake wa kwanza, akiwa na kikosi kipya na benchi jipya la ufundi, ameiongoza Simba SC kufika fainali ya Kombe la Shirikisho la CAF.
“Chini ya Kocha Fadlu Davids, Simba imefika fainali ya CAF Confederation Cup, fainali ya pili ya kimataifa katika historia ya klabu. Msimu huu ulikuwa wa kujenga timu. Na bado tukafika fainali, licha ya upinzani mkali. Simba haitazuilika msimu ujao.”
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.