INAELEZWA kuwa Celestin Ecua ambaye ni kiungo wa Zoman FC huenda akasaini mkataba wa miaka miwili kuwa katika kikosi cha mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara inayodhaminiwa na NBC.
Yanga SC baada ya mechi 30 ambazo ni dakika 2,700 walikusanya jumla ya pointi 82 ikiwaacha watani zao wa jadi Simba SC kwa tofauti ya pointi nne.
Simba SC iligotea nafasi ya pili ikiwa na pointi 78. Mchezo wa Kariakoo Dabi, Juni 25 2025 uliamua bingwa wa msimu baada ya Yanga SC kushinda kwa mabao 2-0 yakifungwa na Pacome kwa pigo la penalti na Clemet Mzize ambaye alitumia pasi ya Pacome.
Inaelezwa kuwa Ecua hueanda msimu wa 2025/26 atakuwa ndani ya Yanga SC akivaa uzi wa njano na kijani kwenye majukumu katika ligi namba nne kwa ubora.
Imeandikwa na Lunyamadzo Mlyuka, Mtunzi kitabu cha Ganzi ya Maumivu Kwenye Upendo, kukipata TUNAOMBA ODA 0756 028 371. Ni simulizi inayozungumzia maisha ya Kiafrika, usaliti, visa, furaha. Wakazi wa Njombe kitabu kinapatikana Mtaa wa Mpechi kwa Chris Jabari, Kigamboni kwa Tupokigwe, Posta karibu na Mnara wa Askari ukiwa unaelekea chuo cha IFM. Kuna kazi mpya inaandaliwa inaitwa Moyo Wangu Unavuja Damu itazinduliwa rasmi Julai 24 2025 usipange kukosa.