MAMELODI SUNDOWNS WABEBA UBINGWA WA LIGI KUU AFRIKA KUSINI KWA MARA YA NANE MFULULIZO

Mamelodi Sundowns ni Mabingwa wa Ligi Kuu ya Afrika Kusini kwa msimu wa 2024/25 kufuatia ushindi wa 3-0 dhidi ya Chippa United usiku huu huku wakifikisha 70 baada ya mechi 27.

Kikosi hicho kinachonolewa na Miguel Cardoso kimetwaa ubingwa wa Ligi hiyo kwa mara ya 8 mfululizo na msimu huu wamefunga jumla ya magoli 63 na kuruhusu mabao 13 tu.

FT: Chippa United 0-3 Mamelodi Sundowns
⚽ 11’ Rayners
⚽ 69’ Arthur Sales
⚽ 89’ Arthur Sales